Taarifa za mabadiliko hayo zilitolewa jana na Mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga ambaye aliwatangazia wabunge katika kikao cha jioni.
Kwa mujibu wa mabadiliko hayo ambayo ni ya tatu tangu Bunge la Kumi na Moja kuanza, Ezekiel Maige amehamishwa kutoka Nishati na Madini kwenda Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), wengine waliohamishiwa PAC ni Allan Kiula kutoka Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Omary Mgumba kutoka Sheria Ndogo, Rhoda Kunchela kutoka Masuala ya Ukimwi na Joseph Kakunda kutoka Kamati ya Uwekezaji.

0 comments:
Post a Comment