Akiwa na miezi saba sasa, bado sura ya Saint West haijulikani kwa wengi sababu ameendelea kumficha ndani.
Na sasa Kim Kardashian ameona ni muda wa kumuonesha mtoto huyo wa kiume kwenye macho ya dunia kwa mara ya kwanza. Kim alionekana kwenye mtoko wa familia Jumanne hii huku kamera za kipindi chao, Keeping Up With The Kardashians zikirekodi matukio yote.
Kim aliongozana na mwanae wa kwanza, North, na watoto watatu wa dada yake Kourtney. Mason, Penelope na Reign kwenye ziara yao huko San Diego. Hiyo ni mara kwanza Saint anaonekana kwa mashabiki ambaye mara chache sana amekuwa akiwekwa kwenye Instagram.
Kutolewa nje kwa mtoto huyo kumekuja baada ya Kim aliyeolewa na Kanye West kudai kuwa mtoto wake ameanza kuongea. Tazama picha zaidi za familia hiyo.
0 comments:
Post a Comment