Meneja Bidhaa wa Dodoma Wine
Warda Kimaro akiongea na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa mvinyo mpya wa
Dodoma Rose. Uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mtaalam wa kutengeza mvinyo wa Dodoma
Rose Erick Schlunz akiwaelezea wageni waalikwa sifa na ladha ya mvinyo huo mpya
uliozinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Meneja Bidhaa wa Dodoma Wine Warda
Kimaro (kulia) akipita kugonganisha glasi na wageni mbalimbali waliohudhuria
uzinduzi wa mvinyo mpya wa Dodoma Rose. Uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es
Salaam mwishoni mwa wiki.
Cheers: Wageni waalikwa
wakigonganisha glasi kufurahia uzinduzi wa mvinyo mpya wa Dodoma Rose. Uzinduzi
huo uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Kampuni
ya Tanzania Distilleries Limited (TDL) kupitia bidhaa yake ya Dodoma Wine mwishoni
mwa wiki imezindua mvinyo mpya wenye rangi ya pinki uitwao “Dodoma Rose Wine.”
Akizungumza
katika uzinduzi huo, Meneja Bidhaa wa Dodoma Wine, Warda Kimaro, alisema, pamoja
na kuwapatia wateja wao mvinyo wenye ladha tofauti, Dodoma Rose pia inapanua
wigo kwa wakulima mkoani Dodoma kuendelea kuwa na soko la uhakika hivyo
kuwawezesha wananchi kiuchumi.
“Ujio
wa bidhaa hii ya Dodoma Rose maana yake ni kuongeza mahitaji ya mali ghafi ya
kutengenezea mvinyo”, alisema Kimaro. Dodoma Rose inapatikana Tanzania nzima
katika ujazo wa 750 ml kwa bei ya rejareja ya Tshs 10,000
Kuzinduliwa
kwa mvinyo wa Dodoma Rose kumeongeza idadi ya mivinyo ya jamii ya Dodoma kufika
minne. Nyingine ni Dodoma Dry Red Wine, Dodoma Dry White Wine, Dodoma Natural
Sweet Wine na sasa Dodoma Rose Wine. “Pamoja na kwamba Dodoma Wine hutengenezwa
hapa hapa nchini lakini ina ubora wa hali ya juu unaokidhi kiwango cha
kimataifa”, alisema Kimaro na kuogeza kuwa kauli mbiu ya Dodoma Rose wine ni onja ladha tofauti.
Alisema
mbali na Dodoma kuwa mji mkuu wa nchi yetu; lakini pia umekuwa maarufu kwa
kuzalisha mvinyo wa pili kwa ukubwa katika Afrika kusini mwa Sahara. “ndiyo
maana ikaitwa Dodoma Wine kuonyesha mizizi yake na kutambua urithi wetu. Dodoma
Wine ilizinduliwa 2010 Na inatengezwa kutoka kwa zabibu bora kabisa zinazolimwa
na wakulima wetu wa Tanzania”, alisema.
Akiongea
zaidi jinsi kampuni ya TDL inavyounga mkono wakulima wa zabibu, Mkurungenzi
Mtendaji wa TDL Devis Deogratius alisema, ‘Wakulima wa zabibu walikuwa na hali
ngumu hapo zamani lakini kupitia miradi tumeweza kuwainua wakulima sio tu
kuwapa soko la uhakika pekee, lakini pia kwa kuwapa ujuzi wa kulima zabibu
kupitia mtaalamu wetu wa kutengeneza kinywaji cha Dodoma Wine Erik Schlunz,
ambaye leo tuko naye hapa’.
Mtengenezaji
wa kinywaji cha Dodoma Wine Erik Schlunz alipata nafasi ya kuwatembeza wangeni
waalikwa na kuwapa uzoefu wa kuonja mvinyo mbali mbali ya Dodoma Wine.
Devis
alisema kuwa kampuni yake imejipanga kutangaza Dodoma Wine sehemu mbalimbali
nchini na hasa kwenye baadhi ya sehemu za starehe na maduka makubwa (supermarket)
ili kuwwaezesha wateja wao kutambua ni mvinyo ngani unaowafaa. Aliongezea kuwa
uzinduzi huu wa Dodoma Rose Wine ni uthibitisho wa mafanikio yanayotokana na
mvinyo wa Tanzania pamoja na wakulima wa zabibu.
0 comments:
Post a Comment