![]() |
| UJUMBE ULIOSAMBAZWA AMBAO MURO AMEUTOLEA UFAFANUZI |
Ule ujumbe wa Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano
wa klabu ya Yanga, Jerry Muro kuwa ameteuliwa na Rais John Pombe
Magufuli kuwa msemaji msaidizi wa Ikulu imezua gumzo kubwa.
Ujumbe huo umesambaa kwenye mitandao kibao ya kijamii
hasa Whatsapp, Instagram na Facebook ukionyesha Muro atakuwa msaidizi wa
Mkurugenzi Msaidizi wa Mawasiliano Ikulu chini ya Gerson Msigwa.
Hata hivyo, Muro amezungumza na SALEHJEMBE usiku huu na kuthibitisha kuwa taarifa hizo ni uzushi mtupu.
“Hakika ni uzushi, kwanza ile akaunti ya Twitter
iliyoanza kusambaza si yangu,” alisema Muro ambaye tayari TFF imetangaza
kumfungia huku ikiwa haijatoa hukumu.
UJUMBE ULIVYO…
USIEMPENDA KAJA!!!!!!!!
BREAKING NEWS
Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
amemthibitisha Ndg Geryson Msigwa kuwa mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu
huku msaidizi wake akiwa ni aliyekuwa msemaji wa Klabu ya soka ya Yanga
Ndg Jerry Cornel Muro.

0 comments:
Post a Comment