Friday, August 5, 2016

Mhe.Tundu Lissu amepandishwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu saa 8:56 mchana kwa tuhuma za uchochezi. Pichani ni baadhi ya viongozi wa CHADEMA, wanachama pamoja na mawakili waliomsindikiza mahakamani hapo.


Wakati huohuo Katibu Mkuu wa Bavicha Taifa Julius Mwita amekamatwa na polisi akiwa Mahakamani hapo alipokwenda na wenzie kumsindiza Lissu.

Wakati huohuo taarifa kutoka Singida zinaeleza kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo limetoa hati ya kukamatwa kwa Tundu Lissu kwa madai ya kutoa lugha ya uchochezi wakati akifanya mkutano wa hadhara mkoani humo jumatano ya August 03, 2016.

0 comments:

Post a Comment