Imeandikwa na Le Mutuz Nation
KAMPUNI ya
Camel Oil imesema uuzwaji wa kiwanja namba 130 kilichoko
Block A, Manzese
jijini Dar es Salaam ulizingatia taratibu zote za kisheria na kwamba hakuna
sehemu iliyoghushi hati
za kiwanja hicho karna
inavyodaiwa. Baada ya kuona utitiri wa habari za nia ya kupotosha ukweli,
Camel Oil wameonelea ni vyema wakaonyesha upande wa
pili wa shilingi.
Akizungumza na
mwandishi wetuofisini kwake
jana, Meneja wa Kampuni hiyo, Mahfoudh Ally, alisema
kampuni yake ilifata taratibu zote za kiubinadamu na kisheria katika kuuza kiwanja hicho baada ya mmiliki
wa awali, Mzee Mohamed Fakhi kushindwa kulipa deni la Sh bilioni 1.4. Huu ulikuwa uamuzi wa
mwisho kabisa baada ya jitihada za muda mrefu, na za msingi zilizogonga mwamba
baada ya ahadi hewa nyingi sana
kutoka kwa mdeniwa,
Mzee Mohammed.
Alisema kabla ya mwaka 2010 kampuni yake
ilifanya biashara kwa muda mrefu na Mzee Mohamed
wa Manzese Filling
Station kuhusiana na kuuza mafuta kwa mkopo kwa
makubaliano kwamba Camel Oil ilipwe kila mwisho wa mwezi. Camel Oil
iliendelea kukipa kituo hicho mafuta lakini mmiliki wa kituo hicho
aliendelea kulimbikiza deni hadi kufikia
Sh bilioni 1.6 na mwaka 2012 aliacha kununua mafuta kwenye kampuni hiyo ya
Camel bila kutoa taarifa yoyote, na Mzee Mohammed pamoja na mtoto wake wakatokomea kusikofahamika.
“Tulifuatilia kujua kwanini kulikuwa
na ukimya wa
muda na tulitaka kujua atalipaje
deni hilo, baada ya muda kadhaa wa kumtafuta tulimpata na tukakubaliana namna ya kulipa
deni hilo. Alitoa hundi ambazo baadhi zilipita na nyingi ziligonga
ukuta kwani hakuwa na hela benki. Kwa mara nyingine akatokomea
kusikojulikana. Jitihada za dhati
ziliendelea kumtafuta
na kumsihi alipe ila palikuwa na kila dalili
ya kushindwa
kulipa deni. Na tulipoona anashindwa kulipa deni tuliomba kushikilia
hati mbili za viwanja vyake kania dhamana,” alisema.
Alisema Mzee Mohamed alikubali mwenyewe kwa maandishi kwamba viwanja
vyake vishikiliwe na Camel Oil karna dhamana ya deni hilo analodaiwa, na
ushahidi wote wa maandishi upo.
Kwa masikitiko Makubwa, Camel walibaini baadaye
kuwa hata viwanja wanavyotaka kuchukua karna dhamana, Mzee
Mohamed alishaviweka dhamana kwenye kampuni zingine ambazo
zinamdai madeni mbalimbali.
Alisema
hati moja ya Viwanja cha kitalu A, kilichopo Manzese ilikuwa inashikiliwa na
Kampuni ya TOTAL iliyokuwa ikimdai Mzee Mohamed Sh. 165,000,000 lakini Camel Oil ilikubali
kulipa deni hilo ili kushikilia hati hiyo kwa makubaliano na Mzee Mohamed
kwamba fedha hizo ziongezwe kwenye deni la awali la Sh.
Bilioni 1.6, ambazo Camel Oil inamdai.
Pia ushahidi wa maandishi upo.
Mahfoudh alisema kwenye mkataba wa kukubali deni iliyosainiwa Septemba mwaka 2010, Mzee Mohamed alikiri kudaiwa na Camel Oil Sh
bilioni 1.6 ambazo alikubali kuzilipa kwa mujibu wa masharti na makubaliano kwenye
mkataba huo, kitu
ambacho hakuonyesha dalili
ya kutekeleza alichokiahidi.
Mahfoudh alisema kwenye
makubaliano ya mkataba huo, Mohamed ambaye ni mdaiwa alikubali kuweka dhamana
kiwanja namba 130 Kitalu A Manzese
chenye thamani ya Sh milioni
850 na kiwanja namba 861 na namba 862 cha Msasani Beach vyenye
thamani ya Sh. 300,000,000.
Katika hatua isiyo
ya kawaida na ya ajabu,
ya kusikitisha na kudhalilisha, hasa kwa mtu mzima na mwenye hulka
kania Mzee Mohammed,
ni kwenda kula kiapo Polisi
pamoja na Ardhi kwamba alipoteza hati za viwanja vyake akiwa na nia mbaya ya
kudhulumu, kufisadi na kuidanganya Serikali mchana kweupe. Hiki
kilikuwa kitendo kibaya na cha kitapeli. Nyaraka zote za ushahidi pia zinaonyesha
kila kitu kinagaubaga.
Kweli
ukistaajabu ya Musa, uatayaona ya Firauni. Baada ya utitiri wa ushahidi
mweupe kabisa bila chenga, imeshangaza sana kuona mzee Mohammed anajiamini na kuzungumza habari
zisizo sahihi. Karna
vile hii haitoshi, baada ya
kugundulika njama zake za kifisadi, Mzee Mohammed alifungua kesi ya kughushi, dhidi
ya Camel Oil. Baada ya muda sio
mrefu, katika muendelezo wa sinema zake, Mzee
Mohammed alikiri mwenyewe
kufuta kesi ya kughushi na akamuandikia barua IGP na DPP na
Camel wakapata nakata. Katika barua
yake, anasema aliamua kufuta kesi ya kughushi, bila ya
kushurutiswa na yeyote, ila pengine nafsi ilimsuta kusema na kufanya matendo
yasiyoendana na hulka pamoja na umri wake. Watu wake wa karibu,
amabao majina yanahifadhiwa, waliiambia Camel Mzee Mohammed aliamini sana uganga na uchawi kuwa kwamba ana uwezo wa kuwafanya Camel
Oil kuogopa au kusahau hilo
deni. Pia hili lilijidhihirisha katika mikutano iliyofata,
Mzee Mohammed kwa kinywa chake aliwatishia wadeni kuwa atajibadilisha
kuwa NYOKA. Wadeni wakamkumbusha kisa cha Nabii Musa katika Quran tukufu, kuwa uwezo huo ni
wa Allah (SW) na hata kania Allah
ataamua kumbadili awe SIMBA, Wadeni hawatachoka kudai haki yao na wana
imani kubwa sana
Allah atajaalia haki
ipatikane.
Mahfoudh
alisema baada ya jitihada zote kufanyika ili Mzee Mohamed alipe deni hilo
ilishindikana na ndipo walipomtafuta dalali kwa ajili ya kuuza kiwanja cha Manzese kujaribu
kufidia deni ambalo
wanamdai.
Alisema Kampuni ya Udalali ya Bilo Star Debt
Collectors ilipewa kazi hiyo na tarehe 3 Julai ilitoa tangazo kwenye
gazeti la Mzalendo kwa ajili ya kuuza kiwanja cha Mzee Mohamed kilichoko
Manzese kama sehemu
ya kufidia deni analodiwa. Ufupi, taratibu zote za msingi na kisheria
zikawa zimezingatiwa.
“Ingawa tulijua hata tukiuza kiwanja kile
hatutapata kiasi tunachomdai ambacho kwa mwaka 2016 kilishapungua na deni
mpaka July 2016 lilikuwa Sh. Bilioni 1.4 lakini tuliamua tu
tuuze angalau tupate kitakachopatikana
kuliko kukosa kabisa maana mdaiwa alionyesha
dalili zote za kushindwa
kulipa deni hilo na alifurukuta katika sinema
na mbinu zisizo za kistaarabu,” alisema
Aidha, alisema mnada wa
hadhara ulifanyika tarehe 9 Julai 2016 na Kampuni ya State Oil ndiyo
ilipata kiwanja hicho kwa kununua
kwa Sh bilioni moja (1,000,000,000)
hivyo kuwa mmiliki halali wa kiwanja hicho namba 130, Block
A Manzese jijini
Dar es Salaam.
Alisema Camel Oil ilifuata hatua zote za kisheria mpaka kuuza kiwanja hicho
na Mzee Mohamed baada ya kuona ameshindwa kulipa deni aliamua kuanzisha
propaganda za kuichafua kampuni hiyo ili ionekane kwamba imemuonea.
“Habari anazoeneza kwamba amevamiwa
kwenye kiwanja chake sio sahihi na hata nafsi yake yeye mwenyewe
inajua kwamba anaeneza propaganda zisizo sahihi kutaka huruma kutoka
kwa jamii maana karna nyaraka zote za kudaiwa kiasi hicho tunazo
na amesaini mwenyewe,
sisi
Tulichukua hati kama dhamana baada ya
yeye mwenyewe kukubali sasa hatujui kwa nini Mzee mzima anahangaika” alisema
Alipofutwa na mwandishi wetu
kuzungumzia mgogoro huo, Mzee Mohamed alisema suala hilo ameshalifikisha kwenye
vyombo vya dola na anatarajia ukweli utajulikana hivi karibuni. Baada ya
kupitia nyaraka zoote za ushindi , mwandishi alishangazwa sana na hizi
propaganda zinazoenezwa bila hofu walawoga kwa Mungu . Hali kadhalika, ajabu ni
kusema Mzee Mohamed hana tena imani na Police na Mahakama , baada ya kutumia
njia mbalimbali anazozifahamu yeye mwenyewe, katika kupindisha ukweli, ila
Mungu si Athumani, njia hizo zote zikaishia ukingoni. Sasa lawama wanatupiwa
Police na Mahakama badala ya kujipanga kulipa amana za watu.
Le Mutuz Nation


0 comments:
Post a Comment