Tiptop Connection
ni moja kati ya lebo za muziki ambazo ziliwahi kufanya poa sana kwenye
game ya music hapa kibongo bongo, lakini ni ukweli usiofichika kwamba
lebo hiyo kwasasa imedrop kiufanyaji kazi kulingana na ilivyokuwa
zamani.
Ni maswali kemkem ambayo yalikuwa yakipelekwa kwenye uongozi wa lebo
hiyo kutoka kwa mashabiki kuhusiana na ujio wa kazi zao mpya na vitu
kama hivyo, lakini kwa sasa tumepenyezewa taarifa kuhusu maswali hayo
kupungua kwa kiasi kikubwa sana.
Ni exclusive kutoka kwa Madee kiongozi wa lebo hiyo
ambaye anadai kuwa brands za mavazi za lebo hiyo zimepunguza kwa kiasi
kikubwa sana maswali kutoka kwa mashabiki kuhusiana na kazi mpya kutoka
katika lebo hiyo.
“Kipindi cha kati watu walikuwa wanapiga makelele kuhusu
Tiptop haipo, Tiptop hamna kitu ambacho kinasikika, zaidi watu wakawa
wanataka nyimbo mpya za Tiptop, lakini zilivyotoka zile Poolover,
T-Shirts, Kofia wamezigombania mpaka wamesahau maswali ambayo walikuwa
wanatuuliza.”
0 comments:
Post a Comment