Wapimaji viwanja na wapimiwa viwanja watuhumiwa kwa RushwaAsoma hadharani muhutasari wa makubaliano YA kutoa viwanja 10 kwa wapimaji kama Asante Aagiza Takukuru kuchukua hatua maamlaka YA Viwanja vya Ndege hawakushirikishwa na Wampongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuingilia kati uwanja wa Ndege ungegawanywa kinyemela
- Mamlaka YA uwanja wa Ndege waeleza Mipango YA kutumia uwanja huo ikiwemo ujenzi wa Chuo cha marubani, viwanda vidogo

- Mkuu wa Mkoa awataka Mamlaka viwanja vya ndege kulipa fidia kwa mujibu wa sheria kuliko uwanja huo kupimwa viwanja
MKUU wa Mkoa wa Mbeya amewaeleza wakazi wa Pambogo kata YA Iyela kuwa alisimamisha umilikishaji viwanja ktk uwanja wa Ndege wa zamani BAADA YA kubaini taratibu zilikiukwa na zoezi zima kughubikwa na rushwa kwa wapimaji viwanja wa kujitegemea

Kutokana na zuio hilo Mamlaka YA viwanja vya Ndege wamekiri kutoshirikishwa ktk zoezi zima wakati wao ndiyo wenye uwanja huo

Mkuu wa Mkoa ameielekeza Mamlaka ya viwanja vya Ndege kuendelea na Mipango b kabambe YA eneo hilo ikiwemo ujenzi Chuo cha marubani, kituo cha kimataifa hali YA hewa na viwanda vidogo na amewataka kuwalipa fidia wote wanaokidhi vigezo vya kulipwa fidia

Ameagiza TAASISI YA kuzuia na kupambana na rushwa kuchunguza na kuchukua hatua kwa wote waliotaka kutoa na kupokea viwanja Kumi kama asante

0 comments:
Post a Comment