Akutana na viongozi wa soko kuwaeleza hatua alizochukua tangu alipopokea risala yao tarehe 31/12/2016
- Kwa ajili ya kushughulikia tatitizo hilo amehusisha ofisi YA Rais , wizara YA Ardhi na wizara YA viwanda na Biashara
- Awataka viongozi kuwa watulivu na amewaomba ushirikiano
- viongozi wa soko Wampongeza na kushangazwa na kasi iliyoanza nayo kushughulikia suala hilo NDANI YA siku MBILI akaanza kuchukua hatua

Mkuu wa Mkoa amekutana na viongozi wa wafanyabiashara wa soko la sido na kuwaeleza hatua alizoanza kuzichukua tangu apokee risala yao tarehe 3/12/2016 katika viwanja vya sido mara mara BAADA YA zoezi la usafi wa kila mwezi kufanyika pamoja na mambo mengine walimuomba Mkuu wa Mkoa kuingilia kati wapatie eneo wanalofanyia biashara sasa waweze kujenga vibanda vya kudumu na vya kisasa ili kuboresha biashara zao

Soko la sido lina zaidi ya wafanyabiashara 3000 wanafanya biashara eneo hilo kwa masharti YA kufanya biashara kwa muda na hawaruhusiwi kujenga vibanda kwa Tofali
Mkuu wa Mkoa amewahidi kushughulikia suala Lao ili lipatiwe ufumbuzi kwa haraka
0 comments:
Post a Comment