Tuesday, January 3, 2017


Huenda mwaka 2017 ukawa wa neema kwa Adele. Muimbaji huyo wa Uingereza anatarajia kufunga ndoa mwaka huu na mpenzi wake Simon Konecki aliyedumu naye kwa miaka mitano kwenye mahusiano.

Imedaiwa kuwa Simon (42) alimvalisha kwa siri pete ya uchumba ya dhahabu Adele (28) mwezi Oktoba mwaka jana. Chanzo cha karibu cha wawili hao kimesema, “A wedding is still very much on the horizon, but where and when haven’t been decided yet.”
Wawili hao watatarajiwa kuishi East Sussex, Uingereza baada ya ndoa yao kwa kuwa ni sehemu ambayo Simon amekuwa akiipenda zaidi.

0 comments:

Post a Comment