Friday, February 3, 2017

Image may contain: 1 person, smiling


Mbunge wa Siha Mhe.Dr.Godwin Mollel amefanikiwa kuidhibiti serikali na kuzuia muswada wa sheria ya madaktari kuwasilishwa bungeni kwa kuwa ulikuwa na mapungufu mengi.


Mbunge huyo ambaye ndiye Waziri kivuli wa Afya, aliongoza Timu kubwa yenye umoja wabunge wa UKAWA na CCM akiwa kama kocha mkuu wa jopo hilo akiwashauri kusimamia misimamo miwili ambayo ni:
1. TATIZO LA AFYA TANZANIA NI ZAIDI YA SHERIA. Hapa aliitaka serikali kuwekeza kwenye Technologia ya Vifaa tiba na utafiti wa SAYANSI ya afya. Dr.Mollel ambaye ni daktari kitaaluma (MD, Muhimbili), alikosoa pia uchumi wa nchi kuendeshwa kwa mawazo binafsi ya viongozi, hali inayoathiri sekta mbalimbali nchini ikiwemo sekta ya afya.

2. SHERIA YA MADAKTARI IWATAMBUE MADAKTARI WASAIDIZI. Hapa Dr.Mollel alijikita katika kuwashauri wabunge kuukataa muswada huo kwani hauwatambui madaktari wasio na shahada yani Maafisa Tabibu (COs) na Madaktari wasaidizi (AMOs).

Dr.Mollel aliwatetea madaktari hao wenye Diploma na Advanced Diploma yaani CO, AMO, na ADO, na kusisitiza kuwa wanastahili kuheshimiwa na kutambuliwa na sheria hiyo kwani wanafanya kazi kubwa sana ya kuokoa maisha ya watu hasa vijijini.

Muswada huo ulikua ukiwaweka CO na AMO kwenye kundi la wataalamu wa afya shirikishi, lakini Dr.Mollel alisisitiza kuwaweka kwenye kundi la madaktari kwa kuzingatia taaluma yao na kiwango cha elimu.

Kutokana na hoja hizi za kitaalamu, Dr.Mollel alifanikiwa kushawishi wabunge wa CCM na Upinzani na kwa kauli moja wakakubaliana nae kuwa wataukataa muswada huo. Kufuatia hali hiyo Serikali iliamua kuondoa muswada huo bungeni kwenda kuufanyia marekebisho.!

0 comments:

Post a Comment