Posted by Williammalecela.com on Friday, February 03, 2017
 |
Mbunge wa Siha Mhe.Dr.Godwin Mollel amefanikiwa kuidhibiti serikali na
kuzuia muswada wa sheria ya madaktari kuwasilishwa bungeni kwa kuwa
ulikuwa na mapungufu mengi.
Mbunge huyo ambaye ndiye Waziri
kivuli wa Afya, aliongoza Timu kubwa yenye umoja wabunge wa UKAWA na CCM
akiwa kama kocha mkuu wa jopo hilo akiwashauri kusimamia misimamo
miwili ambayo ni:
1. TATIZO LA
AFYA TANZANIA NI ZAIDI YA SHERIA. Hapa aliitaka serikali kuwekeza kwenye
Technologia ya Vifaa tiba na utafiti wa SAYANSI ya afya. Dr.Mollel
ambaye ni daktari kitaaluma (MD, Muhimbili), alikosoa pia uchumi wa nchi
kuendeshwa kwa mawazo binafsi ya viongozi, hali inayoathiri sekta
mbalimbali nchini ikiwemo sekta ya afya.
2. SHERIA YA MADAKTARI
IWATAMBUE MADAKTARI WASAIDIZI. Hapa Dr.Mollel alijikita katika
kuwashauri wabunge kuukataa muswada huo kwani hauwatambui madaktari
wasio na shahada yani Maafisa Tabibu (COs) na Madaktari wasaidizi
(AMOs).
Dr.Mollel aliwatetea madaktari hao wenye Diploma na
Advanced Diploma yaani CO, AMO, na ADO, na kusisitiza kuwa wanastahili
kuheshimiwa na kutambuliwa na sheria hiyo kwani wanafanya kazi kubwa
sana ya kuokoa maisha ya watu hasa vijijini.
Muswada huo ulikua
ukiwaweka CO na AMO kwenye kundi la wataalamu wa afya shirikishi, lakini
Dr.Mollel alisisitiza kuwaweka kwenye kundi la madaktari kwa kuzingatia
taaluma yao na kiwango cha elimu.
Kutokana na hoja hizi za
kitaalamu, Dr.Mollel alifanikiwa kushawishi wabunge wa CCM na Upinzani
na kwa kauli moja wakakubaliana nae kuwa wataukataa muswada huo.
Kufuatia hali hiyo Serikali iliamua kuondoa muswada huo bungeni kwenda
kuufanyia marekebisho.! |
0 comments:
Post a Comment