Friday, February 10, 2017

Roger Federer (kulia) akiwa na Andy Murray(kushoto)

Mcheza tennis Roger Federer amekubali mualiko toka kwa Andy Murray wa kushiriki katika tamasha maalum kwaajili ya kuchangisha fedha zitakazowasaidia watoto.


Federer alikukubali mualiko huo kupitia katika mkanda wa video akiwa amevaa vazi sketi maalumu kama ishara ya kuonesha kukubali mualiko huo.

Murray amesema sababu hasa iliyomfanya amualike Federer ni kutokana na uwezo na kipaji kikubwa alichonacho katika mchezo wa Tennis na namna ambavyo amekuwa akicheza na kushinda mataji.
Andy Murray
 
Roger Federer

Katika tamasha lililopita Murray alikusanya zaidi ya £300,000 ndani ya saa 48 tu.

0 comments:

Post a Comment