Monday, February 27, 2017

Ligi Kuu Soka Tanzania bara inataraji kuendelea tena siku ya Jumatano kwa michezo kadha kupigwa.
Mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Young Africans watakuwa wenyeji wa klabu ya Ruvu Shooting katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Michezo mingine inataraji kupigwa mwishoni mwa juma ambapo, Simba SC itakipiga dhidi ya Mbeya City katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Toto Africans itakipiga dhidi ya mbao Mbao FC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza huku Kagera Sugar ikiikaribisha Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Azam FC pia itacheza dhidi ya Stand United ya Shinyanga kwenye Uwanja wa Chamazi.

Katika hatua nyingine Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limerejesha tena mechi za Ligi Kuu kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Jumapili Machi 5, mwaka huu Mtibwa Sugar itaialika Young Africans kwenye uwanja huo katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya Vodacom utachezwa katika Uwanja wa Uhuru ambapo African Lyon itaialika Mwadui ya Shinyanga wakati Ndanda FC itakuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona.


0 comments:

Post a Comment