Monday, February 27, 2017


Meneja wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amesema anadhani sasa mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic ataweza kukaa Old Traford kwa mwaka mmoja zaidi.


Kauli ya meneja huyo imekuja mara baada ya Ibrahimovic, 35, kuiwezesha United kutwaa taji la EFL kwa kuifungia mabao mawili ya muhimu katika ushindi wa mabao 3-2.

Katika mchezo huo wa fainali ulioikutanisha United dhidi ya Southampton katika dimba la Wembley, Zlatan alienda kambani dakika ya 19 na dakika ya 87.

Mourinho amesema hana kawaida ya kumbembeleza mchezaji, hana kawaida ya kumbembeleza mchezaji aongeze mkataba badala yake mashabiki ndio wanatakiwa kumshawishi mchezaji abaki katika klabu lakini inapokuja juu ya sakata la Ibrahimovic ni vema akabaki.

Wakati huo huo Mourinho, aliwahi kuwa Kocha wa Ibrahimovic wakati akiinoa klabu ya Inter Milan, lakini baadae akaihama klabu hiyo na kuelekea nchini Hispania kukipiga katika klabu ya Barcelona mwaka 2009.


Mourinho amesema wakati Ibrahimovic alipokwenda Hipania alijisikia vibaya sana, lakini alipamua kukipiga katika klabu ya Manchester United ni jambo ambalo lilimfurahisha sana.

0 comments:

Post a Comment