Tuesday, February 28, 2017


Mkurugenzi wa Mashule watoto na walemavu katika mchezo wa mpira wa kikapu Charles Misoji amesema ligi ya mchezo wa wa kikapu kwa jiji la Dar es Salaam imekuwa na ushindani mkubwa tofauti na msimu uliopita.

Misoji amesema ushindani umekuwa mkubwa sana na ni vigumu kufahamu ni timu ipi itakayopata ushindi katika michezo inayoendelea, kwani timu shiriki zimeonekana kujipanga kuwania ubingwa.

Katika hatua nyingine misoji amesema maandalizi kwaajili ya ligi daraja la pili yameshaanza huku timu zaidi ya 24 zikitarajiwa kushiriki.


Misoji amesema kwamba katika ligi hiyo viwanja vilivyopo pembezoni mwa mji ndio vitakavyotumika ili kuutangaza zaidi mchezo wa mpira wa kikapu.

0 comments:

Post a Comment