Wednesday, February 8, 2017


Mwenyekiti wa chama cha soka nchini Uingereza Greg Clarke ameweka wazi mpango wake wa kujiuzulu kama serikali ya Uingereza haitamuunga mkono katika jitihada zake za kuunda upya chama cha soka nchini humo.


Clarke aliweka wazi mpango wake wa kujiuzulu usiku wa jana na sasa atasubiri mjadala unaotaraji kufanyika siku ya Alhamisi katika bunge la Uingereza.

Mjadala huo umeandaliwa na Mbnge Damian Collins ambae pia ni Mwenyekiti wa utamaduni, Habari na Michezo nchini Uingereza.

Katika barua yake ya kujiuzulu, Clarke amesema mchezo wa soka nchini Uingereza unahitaji mabadiliko ya hali ya juu lakini amekataa kukiri kwamba Chama cha soka FA kinadhorotesha mchezo wa soka nchini humo.

Clarke amesema sasa inabidi mambo ya soka yaendeshwe kwa uwazi zaidi hususan katika maamuzi ya mambo mbalimbali ili kufanya mchezo wa soka uzidi kusonga mbele.


Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa FA alietangaza nia yake ya kujizulu amesema anafahamu kwamba mabadiliko hayawezi kupatikana kwa urahisi lakini anaamini yatapatikana.

0 comments:

Post a Comment