Monday, February 27, 2017


Shirikisho la soka nchini TFF lipo katika mazungumzo na makampuni ya mitandao ya mawasilino nchini ili kufanikisha mpango wa kuchangisha fedha kwa ajili ya maandalizi ya timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Boys).


Afisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema mpaka sasa mazungumzo hayo yamefikia pazuri na wanaamini mambo yatakapokaa swa kila mtanzania atakuwa na uwezo wa kuchangia fedha kwa ajili ya kuiwezesha timu hiyo ili ifanikishe azma ya kwenda nchini Gabon kupambana vilivyo.

Wakati huo huo ligi kuu ya soka ya wanawake Tanzania Bara hatua ya Sita bora imeanza rasmi jana katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, huku shirikisho al soka nchini TFF likikiri kufurahishwa na mwanzo wa hatua hiyo.

Afisa habari wa shirikisho hilo Alfred Lucas amesema baada ya matokeo ya jana ya mchezo wa ufunguzi, wanaamini timu nyingine shiriki katika hatu aya sita bora zimejipanga vilivyo kwa ajili ya kuuwani ubingwa wa Tanzania bara.


0 comments:

Post a Comment