Roger
Federer amepata ushindi mbele ya Rafael Nadal katika mchezo wa tennis na sasa
amefanikiwa kutinga katika hatua ya nane bora katika michuano ya wazi ya Indian
Wells.
Katika mchezo huo Federer raia wa
Uswis alipata ushindi wa seti 6-2 6-3.
Huu ni ushindi wa tatu mfululizo
kwa Federer hii ikiwa ni mara ya 36 kwa wawili hao kukutana, toka walipokutana
kwa mara ya kwanza katika jiji la Miami miaka 13 iliyopita.
Nadal, 30, alikuwa akimsumbua sana Federer kwa miaka kadhaa katika
michuano mbalimbali lakini kwa sasa kibao kimegeuka na amemshinda katika
michuano kadhaa ikiwemo michuano ya wazi ya Australia.
Mara baada ya kupata ushindi huo Federer amesema amefanya vema katika
mchezo huo na anashukuru kwamba amefanikiwa kutinga katika hatua inayofata.
Sasa atakutana na Nick Kyrgios, toka Australia
ambae yeye amefanikiwa kumfedhehesha Novak Djokovic kwa kumshinda kwa seti 6-4
7-6 (7-3).
Kyrgios, 21, ameonesha kiwango kizuri katika mchezo huo kiwango ambacho
kimempelekea kupata matokeo hayo.
Kinda huyo amezizima ndoto za Djokovic ambae alikuwa anatafuta ushindi
ili aweze kusonga katika hatua inayofata na kutafuta taji katika michuano hiyo
inayoendelea lakini kupoteza kwa seti mbili mfululizo na kuwa amefungwa Kyrgios
2-0 kwani alipoteza pia katika mchezo mwingine uliopigwa huko Acapulco siku 12
zilizopita.
Mara baada ya kupata ushindi huo Kyrgios amesma alikuw a akianzisha vema
mipira na hivyo kutengeneza hofu kwa mpinzani wake. Amesema ushindi huo
umemjenga kisaikolojia na atajitahidi kumshinda kila anaekutana nae mbele yake.
Kyrgios anashika nafasi ya 15 kwa ubora duniani.
Wakati huo huo Mjapan Kei
Nishikori amefanikiwa kupata
matokeo alipocheza dhidi ya Mmarekani Donald Young na kumfunga kwa seti 6-2
6-4, huku katika michezo mingine Pablo
Carreno Busta pamoja na Pablo
Cuevas wakifanikiwa
kusonga mbele.
Mmarekani Jack Sock anaeshikilia nafasi ya 17 kwa ubora amemshinda
Malek Jaziri toka Tunisia kwa seti 4-6 7-6 (7-1) 7-5.
Kwa upande wa wachezaji wawili Jamie
Murray pamoja na Mbrazil Bruno Soares wamefanikiwa
kusonga katika hatua inayofata mara baada ya kupata ushindi wa
seti 7-6 (7-5) 6-4 dhidi ya Jean-Julien Rojer na Horia Tecau.
0 comments:
Post a Comment