Wednesday, March 15, 2017


Kuelekea katika uchaguzi wa kumchagua rais wa shirikisho la soka barani Afrika Kamati ya utendaji ya shirikisho hilo imefikia maazimio mbali mbali kuhusu michuano mbalimbali ijayo.


Katika mkutano huokuelekea katika michuano ya CHAN ya mwaka 2018 itakayofanyika nchini Kenya Serikali ya Taifa hilo imeonekana kujitoa katika kuhakikisha miundombinu kwaajili ya michuano hiyo inapatikana.

Ukaguzi maalum ulifanyika chini ya Makamu wa Rais wa kwanza wa CAF Suketu Patel kati ya February 20 hadi 24, kwa kutembelea viwanja mbalimbali vilivyopo Nairobi, Eldoret, Meru pamoja na Machakos.


Kuhusu fainali za 2017 za AFCON U-17 zinazotaraji kufanyika nchini Gabon. Ombi la viwanja vya Franceville na Port-Gentil limepitisha na sasa viwanja hivyo ndio vitakavyotumika katika fainali hizo zinazotaraji kupigwa kati ya 14 hadi 28 May 2017.

Kuhuus fainali za AFCON U-20 Zambia kamati ya CAF imeitumia Zambia barua kuipongeza serikali pamoja na mamlaka zinazohusika na mchezo wa soka nchini humo kikiwemo Chama cha Mchezo wa soka Zambia FAZ kutokana na maandalizi mazuri walioyafanya.

Katika soka la wanawake ratiba imeshapangwa kwaajili ya mashindano ya 11 ya fainali za wanawake AFCON. Fainali hizo zitafanyika nchini Ghana 2018, kati ya Novemaba 17 hadi December 1 ya mwaka 2018.

Kwa upande wa mtoano pamoja na kuwania nafasi ya kutinga katika fainali hizo za wanawake itakuwa ni kati ya February 26, 2018.

Kalenda kwa soka la wanawake nayo pia imeshaandaliwa kwaajili ya fainali za wanandinga wenye umri cchini ya miaka 20 pamoja na 17.

Katika hatua nyingine kamati hiyo iliiruhusu sekretariet ya CAF kuanza mchakato wa kuitafuta nchi itakayoandaa fainali za Mataifa ya Afrika kwa wanwake ya mwaka 2020.

Maazimio mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na kamati ya maadili kuiuhusu kamati ya nidhamu ya CAF kujadili kesi mbalimbali ikiwemo kesi ya Rais wa COSAFA, ambae pia ni raisi wa Shirikisho la mchezo wa soka Zimbabwe Philip Chiyangwa ambae ameonekana kuishambulia CAF pamoja na kumshambulia Rais Issa Hayatou.

0 comments:

Post a Comment