Timu ya
McLaren imejikuta katika wakati mgumu kwenye michuano ya majaribio kabla ya
kuanza kwa michuano mbalimbali katika mbio za langalanga licha ya mabadiliko
kadhaa yaliyofanywa na Honda ili kuboresha injini za timu hiyo.
Vandoorne samesema yeye pamoja na
dereva mwenzake wangefurahi zaidi kama wangeweza kumaliza mizunguko yote wakati
wa mazoezi, hivyo kwa sasa anadhani ni jambo la busara kwa timu yake kuangalia
namna itakavyoweza kukabiliana na changamoto zilizojitokeza ili zisijirudie.
Katika majaribio hayo, mbelgiji Stoffel
Vandoorne alifanikiwa kumaliza mizunguko 40 tu akiwa amemzidi dereva mwenzake Fernando
Alonso kwa mizunguko 11.
Gari ambalo alikuwa akitumia
dereva Alonso lilipata matatizo kutokana na mfumo wa tanki la mafuta kushindwa
kufanya kazi vema.
![]() |
| Fernando Alonso (kushoto) akiwa na dereva mwezake Stoffel Vandoorne (kulia) |
Honda imetambulisha injini mpya
zenye mfumo wa turbo toka mwaka 2014 wakiwa wamefata falsafa ya timu ya Mercedes.
Siku ya Meneja anaehusika na
maswala ya utengenezaji wa injini toka katika timu ya Honda, Yusuke Hasegawa alisema
kwamba mabadiliko ambayo waliyafanya katika gari lao jipya yangeweza kuleta
ushindani mkubwa lakini sasa imeonekana kuwa kuna baadhi ya kasoro.
Hata hivyo teknolojia iliyohusika
taika utengenezaji huo imeleta mkanganyiko ndani ya Honda kutokana na timu hiyo
kuifanya teknolojia hiyo ifanye kazi ipasavyo ndani ya gari la McLaren Honda.


0 comments:
Post a Comment