Wednesday, March 1, 2017


Mchezaji nambari tatu kwa ubora katika mchezo wa gofu duniani Rory McIlroy amerudidhwa nyuma sana na ukosoaji uliofanya na mashabiki wa mchezo huo pale aipocheza mchezo huo na rais wa Marekani Donald Trump.


Rory, ambae sasa amerejea katika michezo ya PGA inayoendelea nchini Mexico amesema mara baada ya kucheza na bwana Trump ameonekana kuwa ni mtu mwenye kutumia mabavu pamoja na ubaguzi wa hali ya juu.
Akizungumzia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea wakati wakicheza gofu, Rory amesema mazungumzo yao yalijikita katika mchezo wa gofu na hakuna jambo lolote lile la kisiasa walilolijadili.
Licha ya kuwa na kuwa na umri wa miaka 41, Rory bado anashiriki katika mashindano ya mabingwa yaani Masters – na amefanikiwa kushinda mara nne.
Alipoulizwa na wanahabari kuhusu mchezo wake dhidi ya Bwana Trump, Rory amesema alitekeleza agizo hilo kama sehemu ya heshima kwani ingekuwa si rahisi hata kidogo kumkatalia rais kucheza nae gofu.
Amesema hakubaliani nae kwa kila analolifanya katika utawala wake japo yeye si mmarekani na wala hawezi kupiga kura katika chaguzi mbalimbali za Marekani.
Katika hatua nyingine Rory amesema amepata nafasi ya kuonana na aliyekuwa bingwa wa dunia katika mchezo huo mkongwe Tiger Woods, na kusema kwamba hali yake kiafya imeimarika.

Tiger Woods amekuwa akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara katika mika aya hivi karibuni na hajarejea tena viwanjani toka alipojitoa katika mashindano ya jangwani ya Dubai Desert Classic mwezi February.

0 comments:

Post a Comment