Saturday, April 1, 2017

Kufuatia uteuzi wa Bibi Blandina S.J. Nyoni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) tarehe 25/02/2017. Mhe. William V. Lukuvi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 5(2) cha Sheria Na. 2 ya Mwaka 1990, amewateua Wajumbe 7 wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa. 

Aidha, uteuzi huu ni wa kipindi cha miaka mitatu (3), kuanzia tarehe 23 Machi, 2017.

Majina ya wajumbe hao ni kama ifuatavyo: 

Prof. John M. Lupala
Bwn. Gabriel Malata
Bi. Mary Mlay
Bi. Subira Mchumo
Bwn. Ally Hussein Laay
Bwn. Pius Maneno
Bwn. Kesogukwele Masudi Issa Miraji Msita 


Imetolewa na: 

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

0 comments:

Post a Comment