Monday, August 21, 2017

Image result for giraffe images

Itambulike  kwamba Twiga ni mnyama mrefu kuliko wote Duniani.Ni mnyama ambae hupenda amani sana,


Sifa yake ingine Wanyama wenzake hujisikia amani kukaa nae  Akikupiga teke lake likakupata ni Ngumu sana kupona ambapo hata wanyama wenzio huogopa teke hilo. Hupatika Afrika Pekee ambapo upole na utulivu wake humfanya awe mwenye kuvutia sana.

Muda mwingi anautumia kujitafuna anapenda kutalii na kushangaa ulimwengu ulivyo. Hutumia muda mfupi kulala kuliko wanyama wengine. Anauwezo wa kutafuna majani yaliko kwenye miti mirefu zaidi tofauti na Wanyama wengine. Twiga ana moyo mkubwa unaofika kilo kumi

Twiga wa kike hubeba mimba kwa muda wa siku 420 hadi 468.Twiga huweza kuzaa mtoto mmoja kwa mara moja na anaweza kuishi zaidi ya miaka 20 hadi 30 Hubeba mimba kati ya miez 14 hadi 15. Ni mnyama anaevutia kuliko wote  kwa hapa Tanzania.

Binadamu anaweza kupita katikati ya miguu yatwiga kijana bila kugusa mwili wake na bado nafasi kubwa ikabaki.Anatumia miguu ya mbele kama silaha yake wakati wamapigano.Nimyama ambae si mvuvi na ana  madaha. Shingo yake ndie sehemu inayo msimumua kimahaba wanapokutana dume na jike.

0 comments:

Post a Comment