Posted by Williammalecela.com on Monday, August 21, 2017
 |
Haya tunayoyaona kwa Lissu inatuonesha jinsi gani upeo wake upo
kiuanaharakati zaidi kuliko uongozi na katika hili ni kama bomu
linalosubiri kulipuka ambalo hata viongozi wa chama chake na hata
wafuasi wake wanashindwa kuling’amua,” alieleza Dk Ndumbaro.
Maneno ya Dk Ndumbaro yaliungwa mkono ya Mhadhiri mwingine wa Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam, Profesa Haji Semboja ambaye alisema tatizo kubwa la
Lissu ni kukosa maarifa ya uongozi.
“Lissu hajui uongozi na hii ndiyo shida kubwa inayomkabili. Hajui suala
la maslahi ya nchi katika siku zijazo na siku zote amekuwa akiona
mabaya,” alieleza Profesa Semboja.
Kwa upande wake, mtaalamu wa sheria za kodi ya madini, Dk Hellen
Kihunsi alisema hata kama kuzuiwa kwa ndege ni suala la kisheria lakini
Tundu Lissu alipaswa kutumia njia bora zaidi ya kuwasilisha kwa mamlaka
husika badala ya kukimbilia kwenye vyombo vya habari.
“Masuala
kama haya yana maslahi kwa Taifa mbapo hata yeye (Lissu) ni sehemu ya
Taifa hili, lakini kwa mwenendo ambao siku zote amekuwa akiuonesha
unatilia shaka uadilifu na uzalendo wake kwa Taifa,” alieleza Dk
Kihunsi.
Tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze kuchukua juhudi ya
kuifufua Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), kumekuwa na baadhi ya
wanasiasa kutoka vyama vya upinzani wakipinga juhudi hizo, ambapo ndege
mbili za awali aina ya Bombardier zilipigiwa kelele na wapinzani wakidai
hazifai licha ya kwamba zimekuwa msaada mkubwa katika sekta ya
usafirishaji.
|
0 comments:
Post a Comment