Monday, September 4, 2017

  Antonio Conte provides major prediction on Diego Costa future
Mshambuliaji wa Hipsania mwenye asili ya Brazil, Diego Costa anayekipiga katika klabu ya Chelsa amejumuishwa kwenye kikosi cha Chelsea msimu huu licha ya mtafaruku uliopo kati yake na timu hiyo.

Chelsea inaonekana imekubali ayishe na wamemaliza tofauti zao baada ya Mhispania huyo kutajwa katika kikosi cha timu hiyo kinachoshiriki Ligi Kuu England msimu huu.

Mhispania huyo aliweka mgomo na kulazimisha kutaka kurejea Atletico Madrid baada ya bosi wa Blues, Antonio Conte kumtumia ujumbe wa kumtaka aondoke.
Mbali ya Chelsea, pia Liverpool na Arsenal zimefanikiwa kushinda vita zao na wachezaji wao wanaotaka kuondoka Philippe Coutinho na Alexis Sanchez wametajwa katika orodha ya wachezaji 25 watakaowatumia katika msimu.
Coutinho alikuwa akihusishwa kutakiwa na Barcelona kwa muda mrefu, wakati dirisha la usajiki Hispania likifungwa leo usiku bado kuna uwezekano wa kujiunga na miamba hiyo Catalans.
Huku Alexis Sanchez alikuwa na hamu kubwa ya kuondoka Arsenal kujiunga na Manchester City, lakini Gunners ilikataa dau la City la pauni 60milioni.
Costa, 28, yuko nyumbani kwao Lagarto, Brazil na kukosekana kwake mazoezini kwa siku 14 atakuwa akitozwa faini ya pauni 300,000.
Chelsea na Atletico sasa wanaweza kujadiliana kuhusu kumruhusu mshambuliaji huyo kurejea Madrid, japokuwa kikwazo kikubwa ni ada ya uhamisho.
Chelsea inataka walipwe pauni 50milioni kwa mshambuliaji huyo waliyemnunua kwa pauni 32milioni miaka tatu iliyopita.
Categories:

0 comments:

Post a Comment