Posted by Williammalecela.com on Tuesday, September 05, 2017
Kampuni
ya Simu ya Halotel Tanzania wakishirikiana na Finca leo wamezindua
huduma ya Benki ya mkononi (HALO YAKO) ambayo itasaidia huduma za
kifedha haswa kwa maeneo ya Vijijini.
Akizungumza
katika uzinduzi huo Mr. Le Van Dai ambaye ni Mkurugeni Mtendaji wa
Halotel Tanzania amesema huduma hiyo itaweza kukuza uchumi na itaweza
kuboresha maisha ya watanzania. "Tunashukuru
sana uhusiano ambao tumeujenga kati yetu na Finca ambapo miaka mingi
wamekuwa wakitoa huduma za kifedha kwa jamii ya watanzania " alisema Le. Amesema
watu wa vivijini walikuwa na shida ya kufikiwa na huduma ya kifedha kwa
njia ya simu na maendeleo ya kitekinolojia yametoa fursa kwa Kampuni ya
mawasiliano ya simu ya halotel na kushirikiana na Finca Microfinance
Bank. Aidha
huduma ya HALO YAKO inapatika kupitia huduma ya HALOPESA inayotolewa na
kampuni ya Halotel ambayo ni huduma ya kifedha inayomwezesha mteja
kutuma na kupokea fedha kwa urahisi na kwa usalama. Kwa
upande wa Mkurugenzi wa Finca Issa Ngwengwe amesema wameungana na
Halotel kufanikisha huduma hiyo kwa watumiaji na wataweza kuwa na
akaunti ya Bank kwa kutumia simu yake ya mkononi. Mgeni
rasmi kwenye uzinduzi huo ambaye amekuja kwa niaba ya Waziri wa fedha
ambaye ni kamishna wa fedha za nje John Lubuga amesema serikali iko
tayari kushirikiana na kampuni mbalimbali zenye malengo ya kuondoa
umasikini kwa watanzania hivyo wanaipongeza Halotel na Finca.
0 comments:
Post a Comment