Tuesday, September 1, 2015

‪#‎HABARI‬ DR. SLAA AFUNGUKA
 
Dr. katika hoteli ya Serena akiwa na walinzi wake 7, amefika na kuamua kuweka kila kitu wazi kuhusu ukimya wake. Soma hapo chini alichozungumza


Slaa: Kila mtu ana kiu ya kusikia Dr Slaa anasema nini, sijawahi kuona waandishi wengi hivi

Slaa: Wengi mnafahamu sina tabia ya kuyumbishwa, ninasimami a lile ninaloamini, ijulikane kama binadamu sina chuki na mtu

Slaa: Mimi sikuwa likizo kama mlivyoambiwa na wengine. Nimeamua kuachana na siasa tarehe 28 Julai 2015 saa 3 usiku.
Naomba ijulikane kuwa nilishiriki majadiliano ya awali juu ya ujio wa Lowassa ndani ya CHADEMA, ila sikuafiki ujio wake.

Slaa: Mchakato ndani ya CHADEMA ulianza mapema na jina langu lilipitishwa lakini bado sikuitangaza popote.

Slaa: Suala la Msingi ni kuangalia kama ni ASSET au LIABILITY, ASSET kwa maana kwamba anakuja na watu wangapi kwenye chama

Slaa: Tuliambia anakuja na wabunge wanaomaliza muda wao zaidi ya 50 na viongozi wengine toka CCM.

Slaa: Siku zikapita sikupewa majina ya wabunge hao, wenyeviti wa CCM mikoa wala makatibu wakuu.

Slaa: Upotoshwaji kwamba Dr Slaa alikubali toka mwanzo si kweli naomba viongozi wangu waseme kweli.

Slaa: Kamati kuu tumekaa toka saa 9 hadi 12:30 kikao kikavunjika, ikasemwa iundwe kamati ndogo kunishawishi, nikakataa.

Slaa: Niliandika barua ya kujizuru ndani ya kamati kuu kwa mwenyekiti wakati huo akiwa Profesa Safari, ambaye aliichana.

Slaa: Mimi mwanasiasa niliyozoea naamini siasa ni sayansi haitaki uongo, haitaki udanganyifu.

Slaa: Maamuzi yaliyofanywa, yalifanywa na mimi kwa ridhaa yangu mwenyewe.

Slaa: Sisi katika familia yetu tumezoea propaganda hizo, nishasema kama mna ushahidi muulete

Slaa: Nataka niwahakikishie D. Slaa na watoto wake wameendelea kula mihogo kama tulivyoahidi maana pesa imesaidia watanzania

Slaa:Ni lazima mwanasiasa yoyote duniani hataji jina linachafuliwe, hata Dr Slaa hataki jina lake lichafuliwe ni haki yangu.

Slaa: Jambo ambalo nataka nifafanue ni suala zima la LIABILITY au ASSET, ASSET nimelieleza, wamekuwa waongo hawakutekeleza

Slaa: Mtu ambaye hata mwezi mmoja haujapita tangu useme CCM ikimteua Lowassa atajitoa, leo anasema ni msafi.

Slaa: Wenyeviti waliokuja CHADEMA wote toka CCM ni mzigo, makapi.

Slaa: CHADEMA inachukua mtu kwa sifa ya wizi wa kura, kama hatutaki kuiba kura sisi tunaenda kufanya

Slaa: Suala la ASSET sikupata majibu, ndio maana hadi leo viongozi wangu wamepata kigugumizi, naongelea kwanini nimeondoka.

Slaa: Mimi padri , yaani nikubali kuweka mkataba na shetani kwaajili ya kuiondoa CCM? unaondoa CCM kwa 'progamu series

Slaa: Watu waliikubali CHADEMA kwaajili ya misingi ya uadilifu, leo tuna unadilifu?

Slaa: Duniani kote tuhuma zinatolewa na ni jukumu la serikali kutoa majibu. Kama watu hawajui siasa bora wakae kimya.

Slaa: CCM siwezi kuwahurumia, hata Lowassa hapa alipofika ni kwakuwa CCM ilimlea.

Slaa: Kama ukikuta choo cha kitanzania, ukapakua kilichoko ndani ya choo na kuweka chumbani kwako, ipi ni choo?

Slaa: Mimi nilikuwepo 2008 wakati tunajadili RICHMOND tunapozungumza masuala hayo ni kwakuwa tunayajua na tuliyaishi Bungeni

Slaa: Lowassa tunamtuhumu mengi , mimi simtuhumu kwa RICHMOND tu, 2010 mimi nilimwambia atumbie hadharani RICHMOND ya nani

Slaa: Ni afadhali nipotee kwenye siasa Tanzania na duniani kote kuliko kuyumbishwa na misimamo yangu.

Slaa: Mimi nimeletewa rushwa asubuhi, nikamuuliza aliyeleta kama mimi unanipa milioni 500 unazo ngapi?

Slaa: Mwanzo wa RICHMOND lazima urudi kwanza kwenye taarifa ya baraza la mawaziri februari, 2006.

Slaa: Naomba mtambue kwamba suala hili la RICHMOND halikuanzia kwa Kikwete bali lilianzia kwa Mkapa.

Slaa: 2006 feb 10, Waziri mkuu alikuwa Lowassa, sasa leo unapokuja kunambia hakuhusika maanake nini?

Slaa: Ripoti ya Mwakyembe alitoa option mbili, Waziri Mkuu ajipime au Bunge lijadili na kutoa uamuzi, akakimbilia kujiuzulu.

Slaa: Lowassa dakika ya mwisho aliingilia, hakusaini yeye ila aliagiza personal assistance wake akasaini.

Slaa: Watu wanauliza kwanini namsema Lowassa mwenyewe ni kwakuwa anagombea urais wa nchi.

Slaa: Nendeni basi Monduli kwa Lowassa na Karatu mlinganishe wakati nikiwa mbunge, halafu tuone huyu mnayemuita mtendaji.

Slaa: Mnasema habari za shule ya kata, hizi sio zao lake ni upotoshwaji, aseme alibuni wapi wazo hili.

Slaa: Ugomvi wangu na Masha ni kwasababu nilitoka hadharani na kusema Masha umeingilia mchakato wa serikali, nikawa adui.

Slaa: Wakaandika uongo kuwa RICHMOND ni kampuni ya stationary wala sio umeme

Slaa: Waziri Mkuu anajua yote halafu ananyamaza, kama alikuwa hajui ni mzembe, kama ni mzembe hafai tena kuwa Rais wa nchi.

Slaa: Kumbuka Tanesco ni chombo kinachojitegemea, ikaagizwa kusaini mkataba ambao haikujadili, maanake ni nini?

Slaa: CHADEMA tumaini jipya lilijengekea, vijana wanaliamini ninaogopa, kwa masikitiko ninasema sitaki baadaye tufike pabaya

Slaa: Kama CHADEMA leo inafika hatua ya kujaza uwanjani watu kwa mabasi halafu mnasema kuna mafuriko,siko tayari kuwa zezeta

Slaa: Udanganyifu huu wa kujaza watu kwa kubebwa na magari kuja uwanjani wakajaza uwanja walikuwa nao CCM

Slaa: Nimewasikia CHADEMA jangwani, waliyoongea ni sehemu kubwa ya ilani ambayo ilishaandaliwa zamani, hakuna kipya.

Slaa: Kinachoniumiza ni sisi kuwa wabovu zaidi ya CCM.

Slaa: Nataka Lowassa ajue kuwa tunajua, Scotland inatuandikia kuwa achunguzwe kwa paundi milioni 400 alizopeleka marekani.

Slaa: Halafu wanasema nikizungumza eti nitaharibu sifa yangu, wacha iharibike.

Slaa: Mimi nimefundishwa kukemea maovu.

Slaa: Leo anakuja mtu hapa anatuambia nyamazeni? Mimi sitaki kuingia kwenye mambo ya akina babu seya.

Slaa: Leo baadhi ya vyuo vinatumia kesi ya babu seya kufundishia kama kesi ya ulawiti halafu lowaasa anasema ataifuta

Slaa: Nani aliyeagiza maaskari waingie na mbwa pale mwembe chai msikitini? Sumaye huyu huyu aliagiza.

Slaa: Lowassa akili yake ipimwe, kesi ya ulawiti Rais hapaswi kuingilia, anaingilia uhuru wa mahakama

Slaa: Ni afadhali kutokuwa na Rais wa aina hii, Rais ambaye anatumia udanganyifu kwakuwa watu hawajasoma hafai.

Slaa: Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka basi hata jani ulikimbie, inabidi tuhakikishe kwamba tunakuwa makini

Slaa: Alipokuwa Waziri Mkuu haya matatizo yanayotokea leo hayakutokea laa: Mtu aliyesababisha migogoro ya mipaka halafu leo anataka kuwa Rais?

Slaa: Wapo watakaosema ameichana CHADEMA, ameijenga CCM. Ukweli haugawanyiki, kama yameitandika CHADEMA ndio ukweli ulivyo

Slaa: Nimesema sina chama ila mimi ni mtanzania, nitawatumikia watanzania kwa vipawa alivyonipa Mwenyezi Mungu.

Slaa: Nimeombwa kugombea urais kwenye vyama vitano ila nimekataa kwakuwa mimi siamini katika kuhama hama vyama.

Slaa: Mshenga niliyemtaja, alisema kanisa la kilutheri lote linamuunga mkono Lowassa, na maaskofu wa katoliki 30 wamehongwa

Slaa: Sitaenda chama chochote, nimesema sina chama, siasa kwa maana ya chama sina, ila siasa kwa ninayoamini.

Slaa: Sijaja kufanya kampeni leo, nimekuja kuwakumbusha Watanzania wasije wakajuta kama ambavyo tunajuta kwa kosa tulilofanya 2005 na 2010.

0 comments:

Post a Comment