Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini Johnson Minja amesema
Tanzania imepata rais ambae anafanana na watu wake, kwani viongozi wote
wakubwa akiwemo makamu wa rais na waziri mkuuu wameungana na watanzania
wote kushiriki zoezi zima la usafi, ili kupambana na magonjwa ya mlipuko
ikiwemo kipindupindu.
Pia Minja amesema kuwa suala la usafi liwe endelevu kwa watu wote bila
kujali itikadi na kumtaka kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzie, ili
mazingira yawe safi na salama kwa afya ya kila mtanzania na kuongeza
kuwa suala la usafi kwa vitendo linaipa sifa Taifa kwa wageni mbalimbali
wanaokuja kwa ziara za matembezi nchini

0 comments:
Post a Comment