
Gardiner aliyasema hayo alipokuwa kwenye mahojiano maalum na gazeti hili ambapo alipoulizwa kama kuvunjika kwa ndoa yao ndiyo sababu ya mkewe huyo wa zamani kuyumba, alifunguka:
“Chachu ya mafanikio yake huenda ilitokana na nyota zetu kupatana na ndiyo maana mambo mengi yalienda shwari.”
Mwandishi: Una mpango gani kuhusu ndoa tena?
Gardiner: Kimya kingi kina mshindo, subirini kishindo.
Mwandishi: Unajisikiaje kuishi bila Jide?
Gardiner: Najisikia poa tu ila mwanzo nilipoachwa niliumia sana, tena sana mtu wangu.
Mwandishi: Akikuomba msamaha uko tayari kurudiana naye?
Gardiner: Unajua yule wamezaliwa mapacha, kinyota watu kama hao siyo rahisi kujishusha au kuomba msamaha hata pale inapobidi.
Mwandishi: Kuna madai kuwa baada ya ndoa yenu kwenda mrama mmeamua kugawana mali, hili lina ukweli?
Gardiner: Hilo swali naomba nisijibu tafadhali.
CHANZO: RISASI JUMAMOSI -GPL


0 comments:
Post a Comment