Shirika la Umeme Tanzania – TANESCO, limeeleza nia yake ya kutafuta
namna ya kuwabana wanaoendesha shughuli za kuchomelea vyuma kwenye
makazi ya watu ambayo hayajawekewa nguvu kubwa ya umeme ya kuwezesha
kuendesha mashine zao.
Kwa mujibu wa Tanesco, biashara hiyo kwa sasa imezidi kushamiri
kwenye maeneo mengi nchini na wanaoendesha biashara hiyo wamekuwa
hawaombi vibali Tanesco kwa ajili ya kuunganishiwa umeme unaoendana na
nguvu ya mashine zao.
Akizungumza kwenye kikao cha pamoja baina ya wenyeviti, watendaji na
wajumbe wa serikali za mitaa wilaya ya mbagala mkoa wa Tanesco wa Temeka
jijini Dar es salaaam, Mkuu wa Idara ya Mipango Tanesco mkoa wa Temeke,
Injinia Ffrank Chambua amesema watu hao wanasababisha kuwepo na tatizo
la upungufu wa umeme kwenye mkoa huo na kuwataka watendaji hao
kushirikiana na Tanesco kuwabaini ili wachukuliwe hatua.
Baadhi ya wenyeviti, watendaji na wajumbe wa serikali za mitaa wilaya
ya mbagala waliohudhuria mkutano huo, wakizungumza na channel ten
wameitaka Tanesco kuwa na utamaduni wa kushughulikia matatizo au
malalamiko yanayowasilishwa kwao kwa haraka .
Mkoa wa Tanesco Temeke una jumla ya wateja halali elfu sitini waliounganishiwa umeme na Tanesco
0 comments:
Post a Comment