HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH), imeboresha huduma za afya kwa
wagonjwa wa nje ili wapate muda zaidi wa kutibiwa na kupata ushauri wa
daktari katika kliniki mbalimbali.
Uboreshaji huo utasaidia wagonjwa kupata huduma kwa wakati na
kupunguza muda wa kusubiri kupata huduma hata msongamano katika eneo
moja ndani ya hospitali.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Idara ya Huduma
ya Wagonjwa wa Nje, Dk Raymond Mwenesano wakati akizungumza na waandishi
wa habari.
Alisema utaratibu huo utawasaidia wagonjwa wanaokwenda kutibiwa na
kuondoka hususan wale wanaolipia fedha taslimu, wagonjwa ambao ni
wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), bima mbalimbali za
afya pamoja na watumishi ambao kampuni zao zina mikataba na hospitali
kutibu wafanyakazi wao.

0 comments:
Post a Comment