KIWANGO cha Kodi ya Mshahara (PAYEE) kinatarajiwa kushushwa hadi
asilimia 10 katika mwaka ujao wa fedha wakati serikali ikiendelea
kujadiliana na vyama vya wafanyakazi kwa lengo la kuipunguza hadi
kufikia tarakimu moja.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji alisema pia
wanaangalia uwezekano wa kupunguza kiwango kikubwa cha kodi kwa
watumishi waandamizi ambao wamekuwa wakilipa asilimia kubwa kutokana na
mishahara yao mikubwa.
Alisema hayo jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu,
Hawa Chakoma (CCM) aliyetaka kufahamu serikali imejipangaje kutekeleza
Ilani ya CCM ya mwaka 2015 inayolenga kuwapunguzia wafanyakazi PAYE
kutoka asilimia 11 hadi tarakimu moja.
“Baada ya kufikia kiwango hicho cha asilimia 10, serikali itaendelea
kujadiliana na vyama vya wafanyakazi kwa lengo la kupunguza PAYE hadi
kufikia tarakimu moja kutegemea na hali ya uchumi utakavyokuwa
unaimarika mwaka hadi mwaka,” alisema.
Kima cha chini kisichotozwa kodi ni kipato cha mshahara kisichozidi
Sh 170,000. Alifafanua kuwa watumishi waandamizi wanalipa kodi kubwa
kutokana na mishahara yao mikubwa na kwa asilimia kubwa zaidi ya wale wa
chini

0 comments:
Post a Comment