Friday, August 5, 2016

KOSA LA JOYCE KIRIA KUTISHIWA KUWACHWA NA MUME WAKE
****************************************************************
|¦| Ni Kusema Kung'ang'ania UKUTA Kunawafanya Waonekane kuwa ni Nyumbu



Magoiga S. N-Mwanza

Siku za hivi karibuni Joyce Kiria amekuwa mstari wa mbele ktk kupinga waziwazi kampeni ya Mbowe ya UKUTA kupitia mitandao ya kijamii. Mwanamama huyu alienda ambali zaidi kwa kusema kuwa madhara ya mambo hayo yanawaumiza zaidi wanawake na watoto hivyo akawashauri wake na wenzi wa mabunge na viongozi wa Chadema kufikiria upya mpango huo, na kuwaimba akinamama hao kuwashauri waume zao kuachana nao kwa kile alichodai 'hauna tija' kwa taifa .

Joyce ktk maandishi yake yaliyotapakaa kila kona ktk mitandao ya kijamii ameungana na kauli za Lowasa za wanasiasa kutafuta suluhu kupitia mazungumzo na kuacha siasa za harakati kwa maana ya vurugu, fujo na maandamano.

Ikumbukwe kuwa Joyce ni mwanaharakati wa haki za akina mama na watoto, usawa wa kijinsia pamoja na harakati za kuhamasisha umuhimu wa wanawake kujikwamua kiuchumi na kuacha kuwa tegemezi. Vipindi vyake vya Wanawake Live, Dada Jitambue, Bongo Movie, taasisi ya Hawa na Wadada Centre zimejikita ktk kuwasemea wanawake na kuwaunua kiuchumi na kifikra.
Baadhi ya wakosoaji wanaoegemea mlengo wa Mbowe na UKUTA wametumia nguvu kubwa sana kutoheshimu mawazo ya Joyce badala yake wameanza kumshambulia yeye na hata familia yake. Wakosoaji wengi wanaofuata mkumbo wameenda mbali hata kumshutumu Joyce kuwa anatoa Siri za Ndani.

Lakini nimesoma maandiko ya huyu mwanamama hakuna sehemu nimeona ametoa siri yoyote ile ya kifamilia, kuelezea ugumu wa maish kwa familia ya mzazi mmoja siyo kutoa siri bali ni kutabiri uhalisia . 'This is a normal concern for a normal woman who cares about the wellbeing of her family' Kama wewe hujali basi ni ishara kuwa bado hujajua maana ya familia.
Vyama vya upinzani nchini vimekuwa vikihubiri umuhimu wa watu kuwa huru kutoa mawazo yao bila kujari nani yanamuudhi kuyasiki ilimradi huvunji sheria kwa kufanya hivyo.

Tarehe 21/06/2013, Mume wa Joyce Kiria ajulikanaye kama Henry Kilewo, alikamatwa na polisi kwa kosa la kushambulia na mengineyo aliyotuhimiwa kuyafanya ktk uchaguzi mdogo buko Igunga. JOYCE Kiria na watoto wake waliingia barabarani kuandamana kuomba msaada ili afahamishwe alioo mume wake ambaye alikuwa chini yabukinzi wa polisi. Aliandamana mwenyewe na hakuna aliyemsaidia, alitaabika mwenyewe na hakuna aliyemsaidia kuwalea watoto ktk kipindi chote ambacho mume wake alikuwa akishikiliwa na polisi. Hivyo Joyce Kiria anajua machungu ya familia ktk siasa za fujo, vurugu na maandamano. Likijuwa kisa kushauri watu wenye akili waachane na mawazo ya kushika UKUTA?

Je JOYCE Kiria Kupingana na u-Nyumbu Anamuaibisha Mume Wake au Ni Haki Yake Kutoa Mawazo Yake Kuhusu UKUTA?? Hilo swali utalijibu ktk comment zako ktk hii post.

HAYA NDIYO MAMBOYA MSINGI NILIYOYAONA KTK KATIKA MAANDISHI YA JOYCE KIRIA|¦|Je hapo Joyce amekosea nini??

i) Kumuunga mkono Lowasa, kwa kusema kwamba vurugu, maandamano na kuizuia serikali kufanya kazi yake siyo aina ya siasa zinazotakiwa kwa sasa. Pili kwa kusema kuwa Rais ni Magufuli na hakuna haja ya kufika Ukutani. Je hapo Joyce amekosea nini??
ii) Kusema wahusika wapunguze jazba na waachane na Ukuta. Joyce alisema "Nikapata hisia huenda Daddy alitoa ushauri wa kutatua haya mambo kwa mazungumzo lakini hakusikilizwa... Maana huku mtaa wa pili wameshazoea kutishiatishia na kutunatuna muda wote 😢😢 ndo maana tunaitwa chama cha vurugu😭😭 daddy hajazoea hizo kashkash maskini baba wa watu, akaona akaongelee AzamTv 😢😢" Je hapo Joyce amekosea nini??
iii) Joyce anasema Upinzani Usimdharau Mh Rais "Kiukweli 

Viongozi wakuu upinzani ongeeni na Rais kwa upole na unyenyekevu tena kwa Adabu... Hicho ndo kinachokosekana kwenu kabisa minaona... Naamini Rais anapoona bit zenu na majina ya kumkebehi juu "dikteta uchwara" hafurahii kabisa....anafadhaika tunavyomdharau wakati yeye ndo Rais halali kisheria... Badala ya kumdhihaki mngetafuta nafasi mkae nae mumweleze tatizo lililopo na kumuomba arekebishe...navyomjua huyo baba angewaskiliza fastaaaa...." anasema joyce. Je hapo Joyce amekosea nini??
iv) Joyce kusema haiwezekani nchi moja ikawa na marais wawili, na hii ni nyumba ya Magufuli hivyo tusimvuruge, tumuache afanye kazi. Je hapo Joyce amekosea nini??
v) Hayuko tayari kumuona mume wake anaenda kupigwa mabomu na kupata Kilema cha Kujitakia, harafu mzigo uanze kuwa wa familia. Je hapo Joyce amekosea nini??
vii) Yoyce anasema kufuata kila kitu kizembe ndicho kinachwafanya watu wawaone kqma Nyumbu. Je hapo Joyce amekosea nini??

viii)Kutishiwa kuwa afute post yake ya Facebook la sivyo atapewa talaka. Hiki limenifanya nicheke kidogo na kutafakari ikiwa moja ya vigezo vya ndoa ya hawa wawili ilikuwa ni lazima mke afuate kila agizo la mwenyekiti wa chama cha mume wake. Je mke yuko huru kuwaza tofauti na mbowe anavyowaza?? Hapa Ndipo Unyumbu Unapothibitishwa kua upo.

0 comments:

Post a Comment